Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 5 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 50 2016-02-01

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:-
Hospitali ya Kibena inakabiliwa na uchakavu pamoja na upungufu wa madawa:-
Je, Serikali itakarabati hospitali hiyo pamaja na tatizo la upungufu wa dawa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema Wiliam Mgaya Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ukarabati wa majengo yote ya Hospitali ya Kibena unakadiriwa kugharimu shilingi milioni 805.5 katika bajeti ya mwaka 2014/2015. Serikali imefanikiwa kupeleka shilingi milioni 22 ambazo zimetumika kukarabati chumba cha kuhifadhia maiti na kazi hiyo imekamilika.
Mheshimiwa Spika, ili kuendeleza ukarabati huo Serikali katika bajeti ya mwaka 2015/2016 imepanga kutumia shilingi milioni 260, kwa ajili ya ujenzi wa uzio na ukarabati wa chumba cha X-Ray. Hospitali ya Kibena ina uwezo wa kuwahudumia wagonjwa 134,801 lakini idadi halisi ya wagonjwa wanaohudumiwa hospitalini hapo ni 471,613, wakiwemo wagonjwa kutoka Mikoa na Wilaya ya jirani. Serikali katika bajeti ya mwaka 2015/2016, imefanikiwa kupeleka shilingi milioni 77.78, kati ya shilingi milioni 106 zilizotengwa kwa ajili ya ununuzi wa dawa. Mpango wa Serikali uliopo ni kuipandisha Hospitali ya Kibena kuwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe ili dawa zitakazopatikana ziweze kuendana na mahitaji halisi.