Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 15 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 119 2022-04-29

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaugawa Mkoa wa Tanga ili kuongeza ufanisi katika eneo la Utawala Bora?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi Mbunge wa Jimbo la Mlalo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, utaratibu wa kuanzisha Mkoa, Wilaya na Tarafa mpya umebainishwa kupitia Sheria ya Uanzishwaji wa Mikoa na Wilaya Sura ya 397 (The Regions and Districts Establishment Procedure) Act, 2020) na Mwongozo wa vigezo vya Maeneo Mapya ya Utawala wa mwaka 2014.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria hii, hatua ya awali inahusisha kupata ridhaa ya Vijiji, Kamati za Maendeleo za Kata, Mabaraza ya Madiwani ya Halmashauri zilizomo katika Mkoa, Kamati za Ushauri za Wilaya, na Kamati ya Ushauri ya Mkoa Mama. Baada ya hatua hiyo, maombi hayo yanawasilishwa Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa ajili ya uhakiki na tathmini na baadaye kuwasilishwa kwa Mamlaka husika kwa maamuzi kadri itakavyoona inafaa.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais TAMISEMI, haijapokea wasilisho la mapendekezo ya kugawa Mkoa wa Tanga. Hivyo, nashauri taratibu za uanzishwaji wa maeneo mapya ya utawala zifuatwe. Ahsante.