Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 13 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 107 2022-04-27

Name

Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: -

Je, Tanzania inapokea watalii wa aina ngapi kutoka nje na sekta hii inachangia kiasi gani katika Pato laTaifa kwa mwaka?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amour Khamis Mbarouk, Mbunge wa Tumbe, kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Tanzania imekuwa ikipokea watalii mbalimbali kutoka masoko ya Kimataifa ikiwemo nchi za Bara la Afrika, Amerika, Asia na Pasifiki, Ulaya, na Mashariki ya Kati. Watalii hao wamekuwa wakitembelea Tanzania kwa madhumuni tofauti, ikiwa ni pamoja na mapumziko, kutembelea ndugu na jamaa, biashara, mikutano, matukio, na sababu nyinginezo ikiwemo ziara za kujifunza na matibabu.

Mheshimiwa Spika, sekta ya utalii kabla ya mlipuko wa janga la UVIKO - 19 ilikuwa ikichangia wastani wa asilimia 17.2 ya Pato la Taifa, asilimia 25 ya fedha za kigeni, asilimia 60 ya biashara za huduma na kuzalisha ajira takribani Milioni 1.5, ikiwa ni ajira za moja kwa moja na zile zisizo za moja kwa moja.

Mheshimiwa Spika, mlipuko wa janga la UVIKO-19 ulioikumba Dunia mwishoni mwa mwaka 2019 ulisababisha kupungua kwa idadi ya watalii kutoka 1,527,230 mwaka 2019 hadi watalii 620,867 mwaka 2020. Mapato kutoka Dola za Marekani Bilioni 2.6 hadi Dola za Marekani Bilioni 0.7.