Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 13 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 104 2022-04-27

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya ulinzi kutoka Mtwara – Newala – Masasi hadi Songea kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninapenda kujibu Swali la Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Nanyamba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya ulinzi ya kutoka Mtwara – Newala – Masasi hadi Songea yenye urefu wa KM 358, inaambaa na Mto Ruvuma. Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kwa sasa inaendelea kuifungua barabara hii kwa kiwango cha changarawe na ujenzi wa madaraja makubwa na madogo katika mito na mikondo ya maji inayokatisha barabara hii ili iweze kupitika. Kiasi cha kilometa 208 zimefunguliwa na daraja kubwa la Mbangala lenye urefu wa mita 120 mkataba wa ujenzi umesainiwa tarehe 11 Aprili, 2022. Baada ya kuifungua barabara yote Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.