Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 13 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 101 2022-04-27

Name

Mwanakhamis Kassim Said

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Primary Question

MHE. MWANAKHAMIS KASSIM SAID aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzana na Wakazi wa Kijiji cha Dunga – Zanzibar?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu: -

Mheshimiwa spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwanakhamis Kassim Said Mbunge wa Magomeni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, eneo la Kambi ya Dunga 141KJ limejumuishwa katika Mpango wa Miaka Mitatu wa Wizara wa Kutatua Migogoro ya Ardhi wa 2020/2021 – 2022/2023 unaoendelea kutekelezwa.

Mheshimiwa Spika, upimaji na uthamini katika eneo hili ulianza tarehe 19 Aprili, 2022 na umemalizika tarehe 25 Aprili, 2022. Hatua zinazofuata ni kuwasilisha kitabu cha uthamini kwa Mthamini Mkuu wa Zanzibar kwa ajili ya idhini na kisha kuwasilishwa Wizara ya Fedha na Mipango kwa uhakiki na malipo ya fidia. Namwomba sana Mheshimiwa Mbunge avute subira, kwani mchakato umefikia hatua nzuri na Wizara imedhamiria kumaliza migogoro yote ya ardhi kati ya taasisi zake na wananchi.