Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 13 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 100 2022-04-27

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafufua Shule za Msingi za Ufundi Wilayani Hai na kurejesha mfumo wa wanafunzi kufanya mitihani na kupewa vyeti?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Elinikyo Mafuwe Saashisha, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali iko katika mapitio ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 na uboreshaji wa Mitaala ya Elimu ili iweze kuwajengea wanafunzi stadi na ujuzi mbalimbali ikiwemo ufundi utakaowawezesha kuhitimu na kuhimili ushindani katika soko la ajira ndani na nje ya nchi. Mara baada ya mitaala tajwa kukamilika ikiwa ni pamoja na manunuzi ya vifaa na mashine mbalimbali za ufundi, Elimu ya Ufundi itatolewa katika Shule za Msingi na Sekondari. Aidha, utaratibu wa kufanya mitihani ya Elimu ya Ufundi na kupata vyeti utaandaliwa kwa kushirikiana na mamlaka husika kama vile Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET).

Mheshimiwa Spika, pamoja na mapitio ya Sera na Mitaala, Serikali inaendelea kufanya maboresho makubwa katika Chuo cha Ualimu Kleruu pamoja na Chuo cha Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi cha Morogoro (MVTCC) kwa kufanya ukarabati wa miundombinu ikiwemo ujenzi wa mabweni ya wanafunzi kwa lengo la kuongeza fursa ya mafunzo kwa Walimu wa masomo ya Ufundi.

Mheshimiwa Spika, pia Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Mbeya kimeanza maandalizi ya utoaji wa mafunzo hayo katika ngazi ya Stashahada katika Elimu ya Ufundi, (Diploma in Technical Education na Postgraduate Diploma in Technical Education). Kwa sasa mitaala ya masomo hayo inafanyiwa kazi na Tume ya Vyuo Vikuu ili kuidhinishwa na kuanza kutumika katika Chuo hicho. Ahsante sana.