Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 13 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 106 2022-04-27

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itasaidia vikundi vya Uvuvi katika Jimbo la Mtwara Mjini?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Seleman Mtenga, Mbunge wa Mtwara Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuhamasisha wavuvi kuunda vyama vya ushirika pamoja na kuviunganisha na taasisi mbalimbali za fedha kwa ajili ya kupata mikopo ya kuboresha shughuli zao za uvuvi, kukuza uchumi wao binafsi na Taifa ambapo hadi sasa kuna jumla ya vyama vya ushirika 170 nchi nzima. Kati ya vyama hivyo, vitatu viko katika Mkoa wa Mtwara.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara imetoa mkopo wa shilingi milioni nane kwa Kikundi cha Uvuvi cha Kaza Moyo Mtwara kwa ajili ya kununua injini na nyavu. Aidha, kupitia mradi wa unaoratibiwa na Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi kwa maana ya FETA, ufadhili wa UNDP Kikundi cha NASARC cha Mtwara Mjini na Kikundi cha wanawake cha Umoja ni Nguvu na chenyewe ni cha Mtwara Vijijini, vimejengewa jumla ya mabwawa 13 ya kufugia samaki wa maji baridi. Jumla ya wanufaika wa mradi huu ni wananchi 140 kutoka katika Vijiji vya Msanga Mkuu, Kijiji cha Mtawanya, Msijute na Mikindani. Mradi huu una thamani ya bilioni moja. Vilevile mradi umelipia gharama zote muhimu za uzalishaji ikiwemo kununua vifaranga na chakula cha samaki hadi kuvuna.

Mheshimiwa Spika, ahsante.