Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 13 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 98 2022-04-27

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka Vifaa Tiba katika Hospitali ya Ilongero pamoja na Vituo vya Afya vya Msange na Mgori Wilayani Singida?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abeid Ramadhani Ighondo, Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2020/2021 Serikali ilipeleka Bohari Kuu ya Dawa Shilingi Bilioni 34 kwa ajili ya ununuzi wa Vifaa Tiba. Tayari Vifaa Tiba vimeanza kusambazwa kwenye Hospitali 67 za Halmashauri ikiwa ni pamoja na Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Singida ambayo imekwishapokea vifaa vya aina 17 vikijumuisha vifaa vya upasuaji na maabara.

Mheshishimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/ 2023 Serikali imetenga Shilingi bilioni 69.95 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba vitakavyopelekwa kwenye hospitali, vituo vya afya na zahanati zilizokamilika.