Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 13 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 97 2022-04-27

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli utakamilika pamoja na kuhakikisha Kituo hiki kinafanya kazi kama kilivyokusudiwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu, Mbunge wa Jimbo la Kibamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Mabasi cha Magufuli kinachoendelea na ujenzi katika eneo la Mbezi Luis kilianza ujenzi Januari, 2019 kwa mkataba wa miezi 18, hivyo ujenzi ulipaswa kukamilika Julai, 2020.

Mheshimiwa Spika, Mkandarasi aliongezewa muda wa ujenzi hadi Juni, 2022 kutokana na kuchelewa kutolewa kwa msamaha wa kodi wa vifaa vya ukamilishaji wa ujenzi huo.

Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Machi, 2022, kiasi cha shilingi bilioni 53.09 sawa na asilimia 94.73 zilikuwa zimelipwa kukamilisha ujenzi. Aidha, tarehe 14 Machi, 2022, Serikali imetoa msamaha wa kodi na sasa Mkandarasi anaendelea na manunuzi ya vifaa ili kazi ya ujenzi iendelee na kukamilika ifikapo mwezi Juni, 2022. Kukamilika kwa kazi hizo kutafanya kituo hicho kutoa huduma kwa wananchi kama ilivyokusudiwa.