Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 81 2022-04-20

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: -

Je, ni nini kinachelewesha ujenzi wa barabara kutoka kutoka Tabora – Mambali – Bukene hadi Kangogwa ilihali ilishatengewa bajeti?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (ENG.GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninapenda kujibu Swali la Mheshimiwa Selemani Jumanne Zedi, Mbunge wa Bukene, kama ifuatavyo: -

Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Tabora – Mambali – Bukene hadi Kagongwa yenye urefu wa KM 114 umekamilika mwaka 2020. Baada ya kukamilika kwa usanifu na gharama za ujenzi kwa kiwango cha lami kujulikana, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi. Aidha, Serikali imejenga kilometa 9.6 kwa kiwango cha lami kutoka Tabora Mjini kuelekea Mambali.

Mheshimiwa Spika, wakati Serikali ikiendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami, Wizara yangu kupitia TANROADS imeendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hii ili iendelee kupitika wakati wote. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 jumla ya Shilingi Milioni 1,200 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo. Ahsante.