Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 9 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 78 2022-04-20

Name

Jonas Van Zeeland

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa mpaka kati ya Hifadhi ya Wamembiki na Wananchi wa Vijiji vinavyopakana na Hifadhi hiyo?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jonas Van Zeeland, Mbunge wa Mvomero kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Pori la Akiba Wami-Mbiki linapakana na vijiji 24 ambapo vijiji Nane vipo upande wa Wilaya ya Mvomero na vijiji Vitatu vipo upande wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro. Aidha, vijiji 13 vipo upande wa Wilaya ya Chalinze, Mkoani Pwani.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa migogoro hii iliwahi kupitiwa na Kamati ya Mawaziri Nane, Serikali kupitia maamuzi ya Baraza la Mawaziri imeshaanza kutatua migogoro hiyo. Utekelezaji wa uamuzi wa Baraza la Mawaziri ulianza tarehe 05 Oktoba, 2021 kwa Mawaziri wa Kisekta na wataalam kupita katika Mikoa yenye migogoro ikiwemo Mkoa wa Morogoro. Aidha, wataalam kwa kushirikiana na uongozi wa Mkoa na Wilaya husika wamepita katika vijiji vyote 24 vinavyopakana na Pori la Akiba la Wamembiki. Baadhi ya mipaka ya vijiji imeonekana kuwa na muingiliano na Mipaka ya Pori la Akiba la Wamembiki. Kwa kuwa watalaam wa Kamati ya Kitaifa ya Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi bado wako uwandani Mkoani Morogoro suala hilo litapatiwa ufumbuzi kwa kushirikiana na uongozi wa Mkoa na Wilaya husika.

Mheshimiwa Spika, nitoe rai kwa wananchi wa Wilaya ya Mvomero hususani katika vijiji vinavyopakana na Pori la Akiba Wamembiki kuwa wavumilivu na kuheshimu mipaka iliyopo wakati Serikali ikiendelea kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa migogoro hiyo.