Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 74 2022-04-20

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya Singida Mjini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Ramadhani Sima Mbunge wa Singida Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetoa fedha Shilingi Bilioni 3.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida ambapo itakapokamilika Hospitali inayotumika sasa itabaki kuwa Hospitali ya Manispaa.

Mheshimiwa Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 imetenga Shilingi Milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali mpya katika Manispaa ya Singida, ambapo fedha hiyo sasa itatumika kukarabati majengo katika Hospitali ya Mkoa ya sasa ambayo itabadilishwa hadhi kuwa Hospitali ya Manispaa ya Singida. Ahsante.