Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 133 2023-02-10

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA K.n.y. MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kwa kuwa hospitali iliyopo ina hadhi ya kituo cha afya na haikidhi mahitaji?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Meatu ilianza kutoa huduma kwa ngazi ya Kituo cha Afya. Aidha, mwaka 1989 ilipandishwa hadhi na kuwa Hospitali ya Wilaya.

Mheshimiwa Spika, Hospitali hii ni miongoni mwa hospitali kongwe 50 ambazo katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga fedha shilingi bilioni 16.5 ili kufanya ukarabati wa hospitali 19.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali itatenga fedha za ukarabati wa hospitali 31 zilizobakia ikiwemo Hospitali ya Wilaya ya Meatu, ahsante.