Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 7 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 109 2023-02-08

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO K.n.y. MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuwapatia Wananchi maeneo ya kulima kutoka kwenye mapori na Hifadhi ambazo hazina wanyama kwa sasa?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Nkasi ni mojawapo ya wilaya zitakazonufaika na uamuzi wa Baraza la Mawaziri wa kumega maeneo ya hifadhi kwa ajili ya shughuli za wananchi ikiwemo kilimo, ufugaji na makazi. Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi unatakiwa kuandaa mpango wa matumizi ya ardhi ili kukidhi mahitaji ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jumla ya hekta 10,828 zimependekezwa kumegwa kutoka Msitu wa Hifadhi ya Lowasi unaopakana na Pori la Akiba la Lwafi kwa ajili ya shughuli za kilimo, ufugaji na makazi.