Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 7 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 107 2023-02-08

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuimarisha Taasisi ya TAKUKURU katika uwajibikaji wake?

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuhakikisha Wananchi wa Tanzania wanakuwa na maendeleo endelevu, Serikali imefanya yafuatayo katika kuimarisha uwajibikaji wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

i. Kuongeza idadi ya watumishi wa Taasisi ya TAKUKURU ikiwa ni pamoja na kufanya mapitio ya uwajibikaji wa watumishi waliopo;

ii. Kuongeza bajeti ya matumizi mengineyo (OC) ya TAKUKURU kwa asilimia 51.7 kutoka shilingi bilioni 20.54 mwaka 2021/2022 hadi shilingi bilioni 31.16. Aidha, bajeti ya maendeleo nayo imeongezeka kwa asilimia 33.3 kutoka bilioni 1.5 kwa mwaka 2021/2022 hadi bilioni mbili kwa mwaka 2022/2023;

iii. Kuwajengea uwezo watumishi 984 wa TAKUKURU ambapo watumishi 976 walipata mafunzo ndani ya nchi na watumishi nane nje ya nchi;

iv. Kutoa fedha za ujenzi wa majengo ya TAKUKURU katika mikoa na wilaya ambazo hazina majengo kulingana na bajeti itakavyo ruhusu.

v. Kuanzisha program za kusaidia kuzuia zaidi rushwa kama TAKUKURU Rafiki

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikakati hii inalenga zaidi kuisaidia TAKUKURU kuzuia zaidi rushwa na pale inapo bidi itaendelea kupambana na vitendo vya rushwa.