Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 6 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 96 2023-02-07

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapunguza ukubwa wa Msitu wa Mbiwe na kurudisha kwa Wananchi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Masache Njelu Kasaka, Mbunge wa Lupa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Hifadhi wa Mbiwe una ukubwa kilomita za mraba 491 na umeanzishwa kwa Tangazo la Serikali Na. 598 la mwaka 1995. Hifadhi ya Msitu wa Mbiwe ni muhimu kwa uhifadhi vyanzo vya maji, kuhifadhi mimea na wanyama, kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na kivutio cha utalii. Eneo hili pia ni ushoroba unaounganisha mapori ya akiba ya Rukwa - Lukwati, Lwafi na Hifadhi ya Taifa Katavi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na umuhimu huo, Serikali haioni haja ya kupunguza eneo hilo.