Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 6 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 95 2023-02-07

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. HAMISI S. TALETALE aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukuza kilimo cha mazao ya viungo katika Wilaya ya Morogoro Vijijini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hamisi Shabani Taletale, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeandaa mkakati wa kuendeleza mazao ya bustani (National Horticulture Development Strategy 2021 - 2031) yakiwemo mazao ya viungo. Ambapo mazao ya iliki, karafuu, vanilla, pilipili manga, tangawizi na mdalasini ni kati ya mazao ya bustani yaliyopewa kipaumbele katika mkakati huo unaolenga kuongeza uzalishaji wa mazao, kuboresha mazingira ya biashara na kuongeza Pato la Taifa linalotokana na mazao hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Wilaya ya Morogoro Vijijini Serikali kwa kushirikiana na Sustainable Agricultural Tanzania (SAT) inatekeleza mradi wa kuendeleza mazao ya viungo katika maeneo yanayozunguka Milima ya Uluguru (Uluguru Spice Project) kuanzia mwaka 2017. Mradi huu umenufaisha wakulima 1,668 katika vijiji 27 vilivyopo Kata za Tawa, Kibongwa, Konde, Kibungo, Mtombozi, Kisemu, Mkuyuni, Kinole. Vilevile, katika kuimarisha uendelezaji wa mazao ya viungo, Chama cha Msingi cha Ushirika wa Wakulima wa Viungo (CHAUWAVIMU) kimesajiliwa kwa lengo la kuimarisha uendelezaji wa mazao ya viungo (pilipili manga, mdalasini, karafuu, taangawizi, iliki na vanilla) katika Wilaya ya Morogoro Vijijini.