Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 78 2023-02-06

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Kilindi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omari Mohamed Kigua, Mbunge wa Kilindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua hitaji la Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Kilindi. Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi imeshatoa eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 15,760 kwa ajili ya kujenga kituo daraja B, pamoja na nyumba za kuishi askari. Fedha za Ujenzi zinatarajiwa kutengwa kwenye Bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2023/2024; nashukuru.