Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 4 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 53 2023-02-03

Name

Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuwasaidia Wananchi wa Mwera ambao hawakuingizwa TASAF na wanaishi chini ya viwango vya umaskini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zahor Mohammed Haji, Mbunge wa Mwera kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unatekelezwa katika halmashauri 184 za Tanzania Bara na Unguja na Pemba katika vijiji, mitaa na shehia zote 410 (shehia 259 kwa Unguja na 151 kwa Pemba).

Kundi la kwanza la wanufaika wa TASAF waliingia kwenye Mpango mwaka 2014. Hata hivyo, si maeneo yote yalifanikiwa kuingia katika kipindi hicho. Kundi la pili liliandikishwa na kuanza kupata ruzuku mwaka 2021, ambapo Mwera waliandikishwa walengwa 924. Kundi hili ni la Walengwa ambao hawakuwa wamefikiwa katika kipindi cha kwanza na hivyo kukamilishwa kwa asilimia 100 ya idadi ya mitaa, vijiji na shehia zote nchini kuwa na wanufaika wa TASAF ikiwemo Jimbo la Mwera.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.