Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 3 Water and Irrigation Wizara ya Maji 44 2023-02-02

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: -

Je, lini maji yatasambazwa Toangoma, Chamazi, Mianzini, Kilungule, Kiburugwa, Kijichi, Mbagala, Charambe, Kibondemaji na Mbagala Kuu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Jafari Chaurembo, Mbunge wa Mbagala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kata za Toangoma, Chamazi Mianzini, Kilungule, Kiburugwa, Kijichi, Mbagala, Charambe, Kibondemaji na Mbagala Kuu zinapata huduma ya majisafi na salama kupitia vyanzo vya maji ya visima virefu na vifupi. Changamoto iliyopo katika kata hizo ni kuwa baadhi ya maeneo hayajafikiwa na mtandao wa maji.

Mheshimiwa Spika, Serikali imepanga kutumia vyanzo vya visima vya Kimbiji kwa ajili ya kumaliza tatizo la maji katika kata hizo. Kwa sasa, taratibu za kumpata mkandarasi zinaendelea na ujenzi unatarajiwa kuanza katika mwaka wa fedha 2023/2024.