Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 39 2023-02-02

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: -

Je, ni lini adha ya Walimu kukaa chini kwa kukosa Ofisi Shule za Msingi za Maendeleo, Bonyokwa na Kinyerezi JICA itatatuliwa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Jimbo la Segerea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mwongozo wa kuanzishwa kwa shule yoyote ni pamoja na kuwepo kwa jengo la utawala ambalo litawawezesha Walimu kuwa na chumba maalum cha kufanyia maandalizi kabla ya kufundisha (staff room).

Mheshimiwa Spika, Shule za Msingi Maendeleo, Bonyokwa, Kinyerezi JICA na Shule ya Sekondari Kimanga hazina majengo ya utawala ambayo ndio huwa na ofisi ya walimu (staff room) hivyo, baadhi ya madarasa ya ziada yamekuwa yakitumika kama ofisi wakati Serikali ikifanya utaratibu wa kujenga ofisi.

Mhesmiwa Spika, ili kutatua changamoto ya Ofisi za Walimu katika Jiji la Dar es Salaam, Ofisi ya Rais, TAMISEMI tumeielekeza Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya utawala katika shule hizo.