Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 36 2023-02-01

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itabadilisha Sera ya Chanjo kitaifa ili kuwakinga watu wengi zaidi badala ya kutibu mtu aliye na ugonjwa tayari?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Urambo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa, gharama za kutibu ugonjwa wowote ni kubwa zaidi kuliko gharama za Kinga kupitia chanjo, kwa magonjwa yanayozulika kwa chanjo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari Serikali imelifanyia kazi suala hilo kwa kupitia Sheria ya Afya ya Jamii ya Mwaka 2009 kifungu 19 ambapo inawataka wazazi na walezi kuhakikisha Watoto chini ya mwaka mmoja na wajawazito wanapatiwa chanjo ili kuwakinga na magonjwa yanayozuilika na chanjo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kutoa wito kwa wazazi, walezi na wajawazito kuhakikisha wanafika vituo vya kutolea huduma za afya ili kupatiwa chanjo.