Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 29 2023-02-01

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: -

Je, ni nini mkakati wa Serikali kuondoa kero ya ukatikaji wa umeme nchini hasa katika maeneo ya biashara kama Kariakoo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuondoa tatizo la ukatikaji umeme Nchini, Serikali imebuni na imeanza utekelezaji wa Mradi kabambe wa Gridi Imara unaolenga kuboresha upatikanaji wa umeme nchini kwa kufanya uboreshaji mkubwa kwenye miundombinu ya kusafirisha na kusambaza umeme. Katika mradi huo, pamoja na kazi nyingine, jumla ya kilomita zipatazo 3,930 za njia za kusafirisha umeme zitajengwa, jumla ya vituo vikubwa vya kupoza umeme 62 vitajengwa na kilomita zipatazo 2,572 za njia za usambazaji umeme zitajengwa. Katika kutekeleza mradi huu, Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 500 kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutatua changamoto ya upungufu wa umeme nchini, Serikali inaendelea na jitihada za kuongeza uzalishaji umeme kupitia vyanzo mbalimbali kama vile gesi, maji, umeme jua na upepo. Miradi hiyo iko kwenye hatua mbalimbali za utekelezaji. Inatarajiwa kuwa, utekelezaji wa miradi hiyo utakapokamilika, utaondoa kabisa kero ya ukatikaji wa umeme nchini. Ahsante.