Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 27 2023-02-01

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: -

Je, ni lini Vituo vya Polisi vya Tarafa ya Mang'ula na Kidatu vitakarabatiwa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abubakari Damian Asenga, Mbunge wa Kilombero kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uchakavu wa Vituo vya Polisi katika Tarafa za Mang'ula na Kidatu. Jengo la Kituo cha Polisi linalotumika Mang'ula ni mali ya Shirika la Reli Tanzania na Zambia -TAZARA, na jengo la Kituo cha Polisi linalotumika Kidatu ni mali ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania -JWTZ. Mnamo tarehe 22 Novemba, 2021 Halmashauri ya Mji wa Ifakara ilitoa eneo la ekari nne kwa ajili kujenga Kituo cha Polisi cha Mang'ula na tarehe 23 Januari, 2023 uongozi wa Kata ya Kidatu ulitoa eneo la ekari mbili kwa ajili ya kujenga Kituo cha Polisi. Taratibu za upimaji wa maeneo hayo zinaendelea kwa ajili ya kupata hatimiliki ili kuandaa michoro na hatimaye kuomba fedha kwenye Bajeti ya Serikali ya mwaka 2023/2024 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya Daraja C.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe Mamlaka ya Upimaji (Halmashauri ya Mji wa Ifakara) waharakishe upatikanaji wa hatimiliki hizo ili mipango ya ujenzi wa vituo hivyo iweze kuandaliwa, nashukuru.