Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 23 2023-02-01

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupandisha Shule za Sekondari za Mchoteka na Nalasi kuwa za kidato cha tano na kidato cha sita Wilayani Tunduru?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, Mbunge Jimbo la Tunduru, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili shule ya sekondari iwe na hadhi ya kidato cha tano na sita inatakiwa iwe na vyumba vya madarasa viwili kwa mkondo mmoja, matundu ya vyoo manne, bweni, maktaba/chumba cha kusomea, jiko na bwalo la chakula.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa shule za sekondari Mchoteka na Nalasi bado hazijakidhi vigezo vya kuwa na kidato cha tano na sita. Aidha, kwakutambua umuhimu wa shule hizo, Serikali kwa kushirikiana na Halmashauri inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha miundombinu ya shule hizo ili ziwe na vigezo vya kupandishwa hadhi na kuwa za Kidato cha Tano na Sita.