Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 44 2022-04-12

Name

Haji Amour Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makunduchi

Primary Question

MHE. HAJI AMOUR HAJI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itashughulikia suala la mtambo wa kielektroniki ulioharibika kwa zaidi ya mwaka sasa na kusababisha mlundikano mkubwa wa hati za ukaazi katika Idara ya Uhamiaji Zanzibar?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Haji Amour Haji Mbunge wa Pangawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha mwezi Januari, 2020 hadi Juni, 2020 mtambo wa kuchapisha kadi za vibali vya elektroniki vya hati za ukaazi (E-Permit) wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar ulisitishwa na kupelekea kadi za hati za ukaazi 139 kuchelewa kuchapishwa kwa sababu ya hitilafu ya mtambo wa kuchapia kadi za vibali vya hati za ukaazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, huduma za utolewaji wa hati za ukaazi ziliendelea kutolewa kwa wageni kwa kugongewa muhuri katika pasipoti ili kuthibitisha kuwepo kwao kihalali hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuanzia Julai, 2020 huduma za utoaji wa hati za kielektroniki ziliendelea kutolewa ambapo hadi kufikia mwezi Machi, 2022 jumla ya vibali 799 vya hati za ukaazi vya kielektroniki vimetolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)