Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 40 2022-04-12

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA K. n. y. MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Shule nyingine ya Msingi katika Kata ya Ng’ambo Tabora Mjini kwani Kata hiyo ni kubwa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Andrea Kainja Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli shule nyingi za msingi hapa nchini zina wanafunzi wengi wanaozidi kiwango katika shule. Hali hiyo pia ni matokeo ya utekelezaji wa Sera ya Elimu Msingi bila malipo iliyoanza utekelezaji wake mwaka 2016.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata Ng’ambo ina shule moja ya msingi yenye madarasa 17 ambayo yanahudumia wanafunzi 2,408. Aidha, ili kukabiliana na ongezeko la wanafunzi katika Kata hiyo Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kwa mwaka wa fedha 2022/2023 imetenga Shilingi Milioni 50 za mapato ya ndani kwa ajili ya ujenzi madarasa mawili ya shule mpya ya msingi inayotarajiwa kujengwa katika eneo la Kilimani katika Kata hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika mwaka wa fedha 2022/2023 itatenga fedha ya ujenzi wa madarasa katika shule mpya ya msingi eneo la Kilimani kupitia programu ya EP4R.