Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 8 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 71 2022-04-19

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kufufua kilimo cha zao la muhogo katika Mkoa wa Mtwara?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Issa Malapo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ilianzisha Mradi wa Kufufua Zao la Muhogo katika Kanda ya Ziwa Victoria na Kanda ya Pwani ukiwemo Mkoa wa Mtwara mwaka 2015. Awamu ya Kwanza ya mradi huo iliisha mwanzoni mwa mwaka 2021, awamu ya pili imeanza Disemba, 2021 na inategemewa kwisha mwaka 2024. Kupitia mradi huu uzalishaji wa muhogo katika Mkoa wa Mtwara umeongezeka kutoka tani 611,210 kwa mwaka 2016/2017 hadi tani 866,676 kwa mwaka 2019/2020.

Mheshimiaw Spika, kutokana na kuongeza utoaji wa huduma za ugani na uzalishaji wa mbegu za muhogo. Jumla ya vipando bora vya muhogo pingili milioni 30.4 kwa mwaka 2019/2020 hadi pingili milioni 40 kwa mwaka 2020/2021 zenye uwezo wa kutoa mavuno mengi kuhimili mabadiliko ya tabia nchi na magonjwa zilizalishwa na kusambazwa kwa wakulima.