Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 8 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 64 2022-04-19

Name

Ramadhan Suleiman Ramadhan

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN aliuliza: -

Je, mgawanyo wa mapato ya tozo za miamala upoje kwa pande za Muungano na vipi yataboresha huduma kwa upande wa Zanzibar?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ramadhan Seleiman Ramadhan, Mbunge wa Chake Chake, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilianzisha tozo ya miamala ya kutuma na kutoa fedha kwa njia ya simu kwa lengo la kugharamia miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali, ikiwemo ujenzi wa vituo vya afya na madarasa. Utaratibu wa mgawanyo wa fedha za tozo ya miamala kwa pande zote mbili za Muungano unasimamiwa na Kanuni ya saba ya Kanuni ya Tozo za Miamala ambapo fedha zinatoka na miamala inayofanyika Zanzibar huwasilishwa Bodi ya Mapato ya Zanzibar.

Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Februari, 2022 jumla ya shilingi bilioni 231.54 zilikusanywa kwa Tanzania Bara na shilingi bilioni 2.96 kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kwa upande wa fedha zilizokusanywa Zanzibar, mchanganuo wa matumizi yake utatolewa ufafanuzi na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Aidha, kwa Tanzania Bara, fedha hizo zimeelekezwa kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ikiwemo ujenzi wa vituo vya afya na madarasa katika tarafa ambazo hazikuwa na miundombinu hiyo. Ahsante sana.