Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 63 2022-04-19

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayoanzia Mji wa Kakonko hadi Muhange?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Jimbo la Buyungu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Kakonko kupitia Vijiji vya Kinonko, Ruhuru, Nyakiyobe, Gwarama, Kabane hadi Muhange inasimamiwa na mamlaka mbili kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kipande cha barabara kutoka Kakonko – Kinonko – Ruhuru – Nyakiyobe – Gwarama yenye urefu wa kilometa 26 inasimamiwa na TANROADS na kipande cha barabara kutoka Gwarama – Muhange yenye urefu wa kilomita nane inasimamiwa na TARURA.

Mheshimiwa Spika, kipande cha barabara inayosimamiwa na TARURA yenye urefu wa kilomita nane ipo katika hali nzuri kufuatia matengenezo yaliyofanyika katika mwaka wa fedha 2019/2020 kwa gharama ya shilingi milioni 40.88.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, kipande cha barabara hii yenye urefu wa kilomita tano, kiasi cha shilingi milioni 10 imetengwa kwa ajili ya matengenezo ili kuhakikisha huduma za kiuchumi na kijamii zinaendelea kufanyika kwa wananchi kwa kipindi chote cha mwaka.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya barabara za Jimbo la Buyungu kulingana na upatikanaji wa fedha.