Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 9 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 129 2022-11-10

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: -

Je, nini kauli ya Serikali kwa wakulima wa vitunguu maji katika Bonde la Eyasi juu ya upatikanaji wa masoko pamoja na bei ya zao hilo?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuhakikisha mazao yanayozalishwa nchini yanapata soko la uhakika, na kuwa mkulima anapata bei nzuri na kunufaika.

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kupitia Idara ya Maendeleo ya Biashara na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (TanTrade) inaendelea kutafuta masoko ya uhakika ya zao la vitunguu maji vinavyolimwa hapa nchini, ikiwa ni pamoja na vitunguu kutoka Bonde la Eyasi ili kupata bei nzuri itakayo wanufaisha wakulima wa zao hilo hapa nchini. Nakushukuru.