Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 9 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 128 2022-11-10

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaajiri wahitimu wa kada ya mazingira waliomaliza katika vyuo vikuu nchini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asia Abdukarimu Halamga, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuhakikisha wahitimu wa kada ya Mazingira na kada ya Afya ya Mazingira (Environmental Health Officers) wanaajiriwa ili kuimarisha jitihada za kukabiliana na athari za uharibifu wa mazingira.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali ilitoa jumla ya vibali vya ajira 223 kwa kada ya Mazingira katika taasisi zipatazo 124 ambapo utekelezaji wa ajira hizo unaendelea. Aidha, katika mwaka huu wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga nafasi 73 za ajira kwa Wataalam wa Mazingira kwa ajili ya taasisi za Serikali zikiwemo Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa. Hatua za utekelezaji wa ajira hizi zote zinaendelea na zinatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka huu wa fedha 2022/2023.

Mheshimwa Spika, jitihada hizi ni endelevu kutokana na umuhimu wa suala la utunzaji wa mazingira ikiwa ni miongoni mwa mikakati ya nchi na dunia kwa ujumla ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.