Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 127 2022-11-10

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwaongezea mkopo akina mama wajasiriamali wa Mkoa wa Katavi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Martha Festo Mariki, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Halmashauri za Mkoa wa Katavi zimekuwa zikitoa mikopo ya uwezeshaji kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu inayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kuzingatia sheria na kanuni za utoaji mikopo hiyo.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Halmashauri za Mkoa wa Katavi zilitoa jumla ya mikopo ya Shilingi milioni 980 sawa na asilimia 105 kwa vikundi 124 vyenye jumla ya wanufaika 850. Katika mwaka wa fedha 2022/2023 halmashauri za mkoa huo zimepanga kutoa mikopo hiyo yenye jumla ya Shilingi bilioni 1.45 sawa na ongezeko la kiasi cha Shilingi milioni 470.

Mheshimiwa Spika, halmashauri zitaendelea kuongeza kiwango cha mikopo kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kulingana na ongezeko la makusanyo ya mapato ya ndani. Ahsante sana.