Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 120 2022-11-09

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA K.n.y. MHE. SEIF K. GULAMALI aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Choma – Ziba – Nkinga hadi Puge?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika naomba kujibu swali la Mheshimiwa Seif Khamis Gulamali Mbunge wa Manonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa Barabara ya Choma – Ziba – Nkinga hadi Puge yenye jumla ya kilometa 109.56 ambayo inapita katika maeneo muhimu ikiwa ni pamoja na Hospitali ya Ndala na Hospitali ya Rufaa ya Nkinga, Serikali kupitia Wakala wa Barabara nchini TANROAD, imeamua kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika mwaka huu wa fedha 2022/2023 kwa lengo la kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.