Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 106 2022-11-08

Name

Haji Amour Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makunduchi

Primary Question

MHE. HAJI AMOUR HAJI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutunga Sera na Sheria ya Kampuni Binafsi za Ulinzi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Haji Amour Haji, Mbunge wa Pangawe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuwepo kwa Sheria na Sera inayosimamia kampuni binafsi za ulinzi. Kwa sasa Waraka wa Baraza la Mawaziri kuhusu mapendekezo ya kutunga Sheria ya Huduma za sekta binafsi za ulinzi umekamilika na utawasilishwa katika Baraza la Mawaziri kwa ajili ya maamuzi baada ya kupata maoni ya kina ya wadau wa pande zote mbili za Muungano juu ya Rasimu ya Sheria hiyo. Baada ya kukamilika kwa hatua hizo, muswada wa sheria utawasilishwa Bungeni.