Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 23 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 198 2016-05-19

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE.FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:-
Magari yanayobeba abiria nchini yamekuwa yakitozwa faini pindi yanapokamatwa kwa kosa la kujaza abiria zaidi ya uwezo wake badala ya kutakiwa kupunguza abiria waliozidi.
(a) Je, Serikali haioni kuwa kutoza faini na kuacha gari liendelee na safari huku likiwa limejaza ni sawa na kuhalalisha kosa?
(b) Je, Serikali haioni kuwa ikiwashusha abira waliozidi itakuwa imetoa fundisho na kupunguza ajali kwa abiria ambao hupanda gari huku wakijua limejaa?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Usalama Barabani Sura ya 168, kifungu cha 58 ni kosa kwa abiria au mtu yeyote kutokuwa na kiti cha kukaa ndani ya gari la abiria na hivyo mtu huyo atahesabika kwamba amening‟inia ndani ya gari hilo. Mabasi yanatozwa faini kwa kuzidisha abiria yakiwa kituoni na maeneo salama abiria wote waliozidi huteremshwa na kurudishiwa nauli zao na utaratibu wa kuwatafutia mabasi mengine ambayo yana nafasi. Aidha, pale ambapo mabasi haya yalizidisha abiria yakikamatwa katika maeneo ambayo si salama huachwa na kuendelea na safari kisha mawasiliano hufanyika katika vituo vya polisi vilivyopo mbele ili abiria washushwe kwenye maeneo ambayo ni salama kwa abiria.
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi, Kikosi cha Usalama Barabarani imekuwa ikiwashusha abiria waliozidi ndani ya basi hasa pale inapokuwa imeonekana maeneo wanayoshushwa ni salama kwa maisha na mali za abiria hao na kutafutiwa usafiri mwingine.