Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 3 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 27 2022-04-08

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Nyamagana, Keza na Djululigwa vilivyojengwa na wananchi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Ngara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua na kuthamini jitihada na michango ya wananchi katika kujenga vituo vya Polisi nchini. Vituo vidogo vya Polisi vya Nyamagana, Keza na Djululigwa ambavyo viko Wilaya ya Ngara, ni vituo vilivyojengwa kwa nguvu za wananchi. Tathmini imefanyika na kubaini kuwa kiasi cha shilingi 125,000,000 kitahitajika ili kugharamia uwekaji wa mfumo wa umeme na maji, kupiga plasta, kuweka sakafu, dari, milango, madirisha, samani na kupaka rangi. Serikali kupitia Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na wadau inatafuta fedha ili kuweza kumalizia kazi ya ujenzi huo.