Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 3 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 23 2022-04-08

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itarejesha kwa wafugaji mifugo iliyokamatwa na TAWA, TFS na WMA ambapo Mahakama ilitoa hukumu irejeshwe?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Luhaga Joelson Mpina, Mbunge wa Kisesa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Uhifadhi Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009 ni kosa kuingiza na kuchunga mifugo ndani ya Hifadhi. Serikali ina jukumu la kulinda Rasilimali na Maliasili za Taifa, ikiwa ni pamoja na kuzuia uharibifu unaosababishwa na uvamizi wa mifugo ndani ya maeneo ya Hifadhi.

Mheshimiwa Spika, wafugaji wanapokamatwa na mifugo ndani ya hifadhi kesi zao hupelekwa Mahakamani ambapo hukumu hutegemea na maamuzi ya Mahakama. Hukumu inaweza kuwa kulipa faini na kurejeshewa mifugo au kutaifishwa. Endapo kuna wananchi ambao mifugo yao ilikamatwa na Mahakama kuamuru kurejeshewa mifugo yao na hawajarejeshewa, wawasilishe malalamiko yao Wizarani ili yashughulikiwe.

Mheshimiwa Spika, ili kuepukana na migogoro ya wafugaji, Serikali inawaomba wananchi hususani wafugaji kujiepusha kuingiza mifugo kwenye maeneo ya Hifadhi.