Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 17 2022-04-06

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ aliuliza: -

Je, kuna wahanga wangapi wa vitendo vya ukatili nchini kuanzia mwaka 2019 hadi 2022?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Fatma Hassan Toufiq, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, takwimu za matukio ya vitendo vya ukatili nchini vilivyoripotiwa kwenye Vituo vya Polisi kuanzia mwaka 2019 hadi Machi, 2022 ni 27,838 kwa mchanganuo ufuatao: -

Matukio ya kubaka ni 19,726; kulawiti ni 3,260 ambao kati ya hao wanaume ni 3,077 na wanawake ni 183; kuunguzwa kwa moto ni 198 kati ya hao wanaume ni 73 na wanawake ni 125; kutupa watoto wachanga ni 443 kati yao wanaume ni 177 na wanawake ni 266; kipigo ni 4,211 ambao kati ya hao wanaume ni 16 na wanawake ni 4,195.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jumla ya kesi zilizofikishwa Mahakamani ni 21,063 na watuhumiwa ambao wamehukumiwa 14,278. Mashauri mengine yako kwenye hatua mbalimbali za upelelezi pamoja na Mahakamani. Aidha, Serikali inaendela kuiasa jamii kutumia vema taasisi za familia kaya, jumuiya za kidini kuanzia ngazi za vitongoji, vijiji na mitaa ili kudhibiti vitendo vya ukatili katika jamii.