Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 10 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 157 2022-11-11

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza maeneo kutoka kwenye hifadhi katika Jimbo la Igalula ili wananchi wa Igalula wapate maeneo ya kuchungia na makazi kwa kuwa idadi ya watu na mifugo imeongezeka?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Jimbo la Igalula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mwaka 2017 Serikali ilifanya mapitio ya mipaka ya msitu wa Uyui Kigwa - Rubuga uliopo Igalula, Wilaya ya Uyui ambapo hekta 36,709 zilitolewa kwa ajili ya vijiji vya Matanda, Sawmill, Kalemela, Itobela, Ibelamilundi, Isenegezya na Isikizya.

Mheshimiwa Spika, Serikali haioni haja tena ya kumega eneo hilo kutoka kwenye hifadhi kwa ajili ya kuwagawia wananchi kutokana na umuhimu wa hifadhi hii kiikolojia. Aidha, vijiji vinaelekezwa kuandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi ili kuepuka migogoro mipya kujitokeza.