Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 86 2022-11-07

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha pembejeo za korosho kwa msimu wa mwaka 2022/2023 zinapatikana kwa wakati na kwa bei nafuu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Nanyamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mahitaji ya pembejeo za zao la korosho katika msimu wa 2023/2024 ni tani 70,000 za salfa ya unga na lita 3,400,000 za viuatilifu vya maji, mabomba 10,000 na magunia 6,200,000. Wizara kupitia Bodi ya Korosho Tanzania inasimamia upatikanaji wa pembejeo za korosho kabla ya msimu kuanza. Tarehe 15 Oktoba, 2022, Kamati ya Ununuzi wa Pembejeo kwa pamoja ilisaini mikataba na kampuni 14 kwa ajili ya ununuzi wa pembejeo hizo.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Bodi ya Korosho Tanzania inaendelea kuratibu zoezi hilo ili kuhakikisha kuwa pembejeo zinawafikia wakulima kwa wakati na bei itakayopangwa kulingana na mahitaji.