Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 79 2022-11-07

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: -

Je, ni upi mchango wa Serikali Kuu katika ujenzi wa Uwanja wa Kisasa wa Michezo wa Halmashauri ya Mji wa Geita?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa utamaduni, Sanaa na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sera ya Maendeleo ya Michezo ya Taifa ya mwaka 1995 Ibara ya 7(1) mpaka (7), jukumu la ujenzi na uendelezaji wa miundombinu ya michezo ni jukumu la Serikali Kuu, Mamlaka ya Serikali za Mitaa na watu binafsi. Hata hivyo, tunaipongeza Halmashauri ya Geita Mji kwa ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu ambao umefikia asilimia 75. Hivyo napenda kutoa wito kwa halmashauri zote nchini kuiga mfano wa Halmashauri ya Geita Mji kwa kujenga fedha kutoka mapato yao ya ndani kwa ajili ya kujenga na kukarabati miundombinu ya michezo.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ipo tayari kutoa mchango wa ushauri wa kitaalamu katika ujenzi wa uwanja wa kisasa wa michezo unaojengwa katika Halmshauri ya Geita Mji, pale itakapohitajika kama ilivyofanya katika halmashauri kadhaa nchini ikiwemo Halmashauri ya Chalinze, Tunduma, Ruangwa na Taasisi kama vile Bandari na Gymkhana. Ahsante.