Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Works, Transport and Communication Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji 73 2022-11-07

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Simiyu utaanza baada ya kukamilika zoezi la uthamini wa eneo la Uwanja utakapojengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kiwanja cha Ndege cha Simiyu kilifanyiwa Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina kwa ufadhili wa Benki ya Dunia mwaka 2017 kupitia Mradi wa
Transport Sector Support Project (TSSP).

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali imekamilisha uthamini kwa maeneo na mali zitakazoathiriwa na utekelezaji wa mradi na kuandaa jedwali la uthamini ambalo tayari limeidhinishwa na Mthamini Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kuendelea na taratibu za malipo.

Mheshimiwa Spika, mara baada ya taratibu za kulipa fidia kukamilika, mipango ya ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Simiyu itaanza kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.