Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 72 2022-11-07

Name

Toufiq Salim Turky

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpendae

Primary Question

MHE. AMINA ALI MZEE K.n.y. MHE. TOUFIQ SALIM TURKY aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuiwezesha TASAC iweze kuhudumia meli nyingi?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Toufiq Salim Turky, Mbunge wa Mpendae, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kuiwezesha TASAC kuhudumia meli nyingi, Serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuongeza watumishi wa ukaguzi wa meli kutoka watumishi 23 hadi watumishi 34. Watumishi walioongezwa wamepelekwa mikoa yote yenye kuungana na bahari na maziwa. Aidha, katika kuboresha uwezo wa wakaguzi, TASAC imepata mkaguzi wa michoro na ujengaji wa meli (naval architect) na imepeleka mkaguzi mmoja kwenda kusomea uchoraji na ujengaji wa meli nchini Uingereza.

Mheshimiwa Spika, TASAC pia imeingia makubaliano na Chuo cha International Maritime Safety, Security and Environment Academy kilichopo Nchini Italia ili kupatiwa mafunzo ya ukaguzi kwa meli za ndani na meli za nje (Flag State Inspection and Port State Inspection). Ahsante.