Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 49 2022-11-04

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati wa kukarabati barabara zilizo katika hali mbaya Wilayani Kyela kwani bajeti ya TARURA haitoshi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Ally Anyigulile Jumbe Mlaghila, Mbunge wa Jimbo la Kyela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kunusuru barabara ambazo zipo katika hali mbaya sana Wilayani Kyela, Serikali imeweka mikakati ifuatayo: -

(i) Kuzipandisha hadhi barabara za udongo kwenda changarawe (Gravel standard);

(ii) Kuzipandisha hadhi barabara za changarawe kuwa barabara za lami;

(iii) Kuendelea kuongeza fedha kwa ajili ya matengenezo na ukarabati wa barabara, mfano, bajeti ya TARURA Kyela kwa mwaka 2020/2021 ilikuwa Sh.611,136,079.47; mwaka 2021/2022 bajeti ya Kyela ilikuwa ni Sh.2,436,996,341.18; na

(iv) Kuendelea kutoa fedha za dharura kunusuru barabara zilizoathiriwa na mvua, mfano, katika mwaka 2021/2022 zimepelekwa milioni 901.52.

Mheshimiwa Spika, fedha zinazopelekwa kwa maelekezo maalum ni kwa ajili ya kutatua changamoto za muda mfupi za barababara zilizoathiriwa na mvua ili ziweze kupitika kwa wakati huo.