Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 19 2022-11-01

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Vitongoji ambavyo havijafikiwa na huduma ya umeme katika Kata za Businde, Bugara na Kibale?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Sebba Bilakwate, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati ambaye ni Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kyerwa ina jumla ya kata 24. Kati ya Kata hizo, kata 21 tayari zina umeme na kata tatu ambazo ni Businde, Bugara na Kibale zenye vijiji 11 zitapata umeme kupitia Mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili (REA III Round II). Kwa sasa, mkandarasi yupo kwenye Kata hizo anaendelea na kazi ya kusambaza umeme katika vijiji 11 kati ya vijiji 29 vilivyopo kwenye wigo wa mradi huu kwa Wilaya ya Kyerwa.

Mheshimiwa Spika, Kata hizo zina jumla ya Vitongoji 62 na tunategemea Vitongoji 33 vitafikiwa na umeme awamu hii na Vitongoji vitakavyobaki vitafikiwa umeme kupitia miradi ya ujazilizi.