Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 1 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 16 2022-11-01

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza: -

Je, ni kwa nini Mfumo wa Stakabadhi Ghalani hautekelezwi kikamilifu kiasi cha kuwawezesha Wakulima kupata fedha wanapohitaji?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Joseph Kizito Mhagama, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mfumo wa Stakabadhi za Ghala unawezesha wakulima kuuza mazao yao kwa bei ya ushindani, wanunuzi kupata mzigo wenye ubora pamoja na Halmashauri kupata takwimu halisi za mauzo na mapato. Katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba zao la kahawa, ufuta na korosho ni baadhi ya mazao ambayo huuzwa kupitia mfumo huo. Mfumo huo, umekuwa na changamoto mbalimbali zikiwemo baadhi ya wanunuzi kuchelewesha malipo kwa wakulima.

Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na changamoto hiyo Serikali itaimarisha usimamizi wa mwongozo unaoainisha muda maalumu wa kuwalipa wakulima kwa kuchukua hatua za kisheria kwa wanaokiuka taratibu.