Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 10 2022-11-01

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kuiwezesha TTCL kuunganisha Wateja wengi kwenye Mkongo wa Taifa kwa punguza gharama za kuunganisha?

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Charles Stephen Kimei, Mbunge wa Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mwezi Septemba, 2021, Wizara iliingia mkataba wa ushirikiano na TANESCO kwa ajili ya matumizi ya pamoja ya miundombinu inayojengwa. Kupitia mkataba huo, miundombinu inayojenjwa kwenye nguzo za TANESCO nchi nzima zinazojumuisha nyaya za mawasiliano zitatumiwa kwa pamoja. Hivyo, kupitia ushirikiano huo, utawezesha TTCL kuunganisha wateja maeneo ya biashara na nyumbani (fiber to X) kwenye Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kwa gharama nafuu kwa kuwa gharama za uwekezaji zitapungua. Aidha, Serikali inaongeza uwezo wa mkongo wa Taifa wa mawasiliano kutoka kiwango cha 200G hadi 800G. Kuongezeka kwa kiwango hiki kitasaidia kupunguza gharama, hali itakayopelekea kuwaunganisha wateja wengi zaidi.

Mheshimiwa Spika, mkakati mwingine wa Serikali ni kuondoa Wizarani shughuli zote za mkongo wa Taifa wa mawasiliano na kupeleka TTCL. Suala hili litawezesha TTCL kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi ya kibiashara kwa haraka zaidi inayojumuisha masuala ya kuwaunganisha wateja kwenye mkongo huo. Aidha, Serikali inaongeza kiwango cha internet band width kinachotumiwa na taasisi 312 za Serikali, taasisi za utafiti na elimu ya juu kutoka 2.1G kwenda 20G. Hii itapunguza gharama za internet kwa taasisi hizo pamoja na nyingine zitakazounganishwa.