Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Madini 3 2022-11-01

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: -

Je, ni maeneo gani yametambuliwa kuwa na madini Mkoani Iringa?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ritta Enespher Kabati (Mbunge wa Viti Maalum) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Taasisi yake ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), ilifanya utafiti wa awali na kuanisha madini yanayopatikana katika Mkoa wa Iringa. Miongoni mwa madini yanayopatikana katika Mkoa wa Iringa ni dhahabu katika Kata za Sadani, Ikweha, Malengamakali, Mlolo, Ifunda, Kalenga, Idodi na Pawaga; shaba katika kata za Mahenge, Kiwele, Pawaga, Nyang’oro, Malengamakali na Kihongota; madini viwanda aina ya chokaa katika Kata za Kiwele, Idodi, Inyigo, Ifunda na Kihongota; udongo wa mfinyanzi (ball clay) katika Kata za Ifunda na Rungemba; kaolin katika Kata za Mbalamaziwa, Nyanyembe, Nyololo na Ifunda; kyanite katika Kata ya Mlowa; bauxite katika Kata ya Rungemba; chuma katika Kata ya Mawindi; na vito katika Kata za Isimani, Idodi na Kiwele.