Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 2 2022-11-01

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga shule mpya za msingi katika maeneo ya Mbirani, Makibo, Kiyombo na Tutuo – Sikonge?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph George Kakunda, Mbunge wa Jimbo la Sikonge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais-TAMISEMI inakamilisha tathmini ya upembuzi yakinifu wa Shule zote za msingi kupitia mradi wa Boost ili kubaini taarifa za eneo shule ilipo, hali ya mazingira shule ilipo, umbali kutoka shule moja hadi nyingine, umbali kati ya shule na makazi ya watu na idadi ya watu (School Mapping). Lengo lake likiwa ni kuandaa mpango endelevu wa uboreshaji wa elimu nchini.

Mheshimiwa Spika, baada ya uhuishaji huo, kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kupitia mradi wa Boost Serikali imetenga Shilingi Bilioni 230 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya shule za msingi katika Halmashauri zote 184 ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge.